Friday, 11 May 2018

UTURUKI YAIAMBIA UFARANSA: QURAN ITALINDWA MPAKA MWISHO WA DUNIA

Msemaji wa ikulu ya rais Uturuki Ibrahim Kalın amepeperusha ujumbe katika ukurasa wake wa Twitter  akifahamisha kuwa kitabu kitakatifu cha uislamu Quran kitalindwa hadi siku ya mwisho dunia itakapotanduka.
Uturuki imejibu na kukemea vikali  hatua ya  baadhi ya  watunzi wa vitabu na wanasiasa nchini Ufaransa waliosaini kuwa baadhi ya aya katika kitabu kitakatifu cha Quran  ziondolewe wakidai kuwa zinazagaza  uhalifu na chuki dhidi ya wayahudi.

Zaidi ya wanasiasa na watunzi wa vitabu zaidi ya 300 nchini Ufaransa  wametia saini wakidai kuwa aya  hizo ziondolewe katika Quran.  Msemaji wa ikulu ya rais wa Uturuki amesema kuwa  Quran ni kitabu kitakatifu na sio kitu cha kufanyia mchezo na kitalindwa hadi siku ya mwisho.

Chuki dhidi ya wayahudi ni fikri na chuki iliapandikizwa barani Ulaya na iwapo Ulaya inataraji kutatua  suala hilo basi ijitathmini na kujiuliza kuhusu historia yake amesema Ibrahim Kalın.

Kwa upande wake  waziri wa mambo ya nje wa Uturuki Mevtlüt Çavuşoğlu  amesema kuwa jambo hilo nchini Ufaransa linaashiria ni kiasi gani chuki dhidi ya uislamu na ubaguzi vinazidi kukita mizizi Ulaya. Waziri wa mambo ya nje wa Uturuki amesema kitando hicho ni uvukwaji wa mipaka.

Historia inaonesha wazi kuwa  wayahudi waliangamizwa barani Ulaya wakati ambapo Utawala wa Dola ya Uthmania na waislamu ulikuwa ukiwapa hifadhi na kuwalinda.

Uislamu hauna chuki dhidi ya wayahudi kwa kuwa ni kinyume na  mafunzo ,  chuki dhidi ya wageni, ubaguzi wa rangi na mabaya mengine vimezidi kuongezeka  barani Ulaya ikiwemo pia vyama vya kibaguzi.