Watu waliokuwa na visu wamevamia mskiti unaopatikana KwaZulu Natal na kuwajeruhi watu wawili na kummalizia maisha mtu mmoja katika shambulizi lao.
Watu hao wawili waliojeruhiwa wamepelekwa hospitali wakiwa katika hali mbaya mno.
Tukio hilo limeripotiwa kutokea Alhamisi kama ilivyofahamishwa na Polisi ambayo imefahamisha kuwa watu hao waliokuwa wamevamia kwa visu walijaribu kuwachinja watu watatu.
Uchunguzi wa polisi unaendelea na bado wahusika wa shambulio hilo hawajatiwa nguvuni wala kubainika chanzo ni nini.