Kitengo kinachohusika na masuala ya dini cha Uturuki Diyanet kimetoa msaada wa Qurani kwa waislamu nchini Uhispania.
Diyanet imetoa kopi za Qurani 3,000 kwa waislamu wa nchini Uhispania.
Qurani hizo zilizotolewa zimetafsiriwa kwa lugha ya kihispania pamoja na lugha ya kiarabu.
Msaada huo umetolewa kwa waislamu wa Granada na Seville.
Kitengo hicho cha masuala ya kidini kimetoa kopi za Qurani zaidi ya milioni moja katika maeneo tofauti ulimwenguni ikiwemo katika mataifa ya Amerika ya Kusini na Asia Mashariki.