Monday, 13 November 2017

WANAWAKE WA KIISLMAU MALAWI WAFANYA IJTIMAHI

Maelfu ya wanawake wa kiislamu nchini Malawi Jumamosi walikusanyika kwenye Ijtimahi lililofanyika Mchinji katika viwanja vya shule ya sekondari ya Bua.

Gertrude Mutharika akisalimiana na viongozi wa kiislamu
Ijtimahi ya namna hiyo hufanyika kila mwaka kwa wanawake wa kiisalmu wa malawi kwa lengo la kusaidia maendeleo ya kufahamu dini yao na mambo mengine yanayohusu
wanawake.

Mgeni rasmi katika Ijtimahi hiyo alikuwa mke wa Rais wa Malawi Gertrude Mutharika ambapo alisema wanawake husaidia sana maendeleo ya nchi.

kinamama wa kiislamu wakiwa katika Ijtimahi
Alisema, "Ili nchi iweze kuendelea, inahitaji ushiriki wa wanawake katika nyanja zote akiwa katika dini ikiwemo shughuli za maendeleo na kutunza familia".

Aliongeza kusema kuwa, "Nafurahi kwamba uislamu humchukulia mwanamke kama sehemu muhimu na wanawake wanapaswa kujifunza kutoka kwa kila mmoja katika Ijtimahi hii".
Gertrude Mutharika akisalimiana na kina mama wa kiislamu
Mutharika pia aliwaomba wanawake kutunza masuala yao ya afya kwa pamoja na mambo mengine, kuhakikisha kuwa wanaenda kufanya uchunguzi wa kansa ya kizazi na kuhudhuria huduma za kabla ya kuzaa ili kuzuia matatizo ya uzazi.

Katika Ijtimahi hiyo Mama Mutharika alivaa vazi la heshima kwa mwanamke wa kiislamu la baibui na hijabu.