Friday, 3 November 2017

AL-HABIB UMAR KUWASILI TANZANIA KESHO SAA KUMI JIONI

Mwanazuoni Mkubwa duniani Alhabib Umar bin Salim bin Hafidh kesho Alasiri anatarajiwa kuwasili katika ardhi ya Tanzania.

Imeelezwa Al-Habib Umar bin Hafiz عمر بن حفيظ  anakuja Tanzania kwa mwaliko wa Mufti wa Tanzania Sheikh Mkuu Abubakar Zubeir na atakaa kwa siku chache kabla ya kuondoka kuelekea nchini Kenya.

Al-Habib Umar bin Hafiz عمر بن حفيظ
Alhabib Umar siku ya jumapili asubuhi kuanzia saa tatu mpaka saa saba mchana atakuwa kwenye ofisi za Bakwata(kinondoni Muslim) na baadae saa tisa mpaka saa kumi atakuwa katika viwanja vya Shule ya sekondari Alharamain iliyoko Kariakoo Shaurimoyo.

Ujio wa Alhabib Umar ni jambo kubwa ambalo waislamu wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kwenda kumpokea katika uwanja wa ndege wa Dar es salaam.

Al-Habib Umar bin Hafiz عمر بن حفيظ ambaye ndiye Mkuu wa chuo cha Dar Al Mustafa kilichoko Tarim, Yemen, inaaminika mbali na Usomi wa dini aliokuwa nao pia ni mchamungu wa kikweli.