Saturday, 11 March 2017

KAMPUNI YA NIKE YATENGENEZA HIJABU KWA WANARIADHA WA KIKE WA KIISALMU

Kampuni  ya Nike inayotengeneza  mavazi na bidhaa mbali mbali za michezo sasa imeanza kutengeneza  hijabu kwa ajili ya wanariadha wanawake wa kiislamu .
Hijabu hizo zinazotambulika kwa jina la 'Nike Pro Hijabs' zimetengenezwa kwa kitambaa imara na cha kudumu .

Hijabu hiyo kwa sasa inatarajiwa kuwa na rangi ya nyeusi na nyeupe na zitaonyeshwa na kuingizwa sokoni majira ya kipupwe mwaka 2018.

Kampuni ya Nike ilitangaza kuwa hijabu hizo zitatengenezwa kwa wingi kulingana na utendaji bora .