![]() |
| Ahmed Al Tibi |
Al tibi wakati anapiga Adhana, wabunge wengi walisimama huku wakipiga kelele za kumtaka Spika amzuie kuendelea kufanya hivyo.
Hata hivyo Al-Tibi aliendelea mpaka kumaliza na kusoma dua baada ya Adhana na kwenda kukaa katika nafasi yake.
"Sheria hii inaonesha kukua kwa ufashisti ndani ya Israel na vitongoji vyake" alisema Tibi.
Pia alimshutumu Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwamba yeye ndiye aliyesimamia muswada huo mpaka kufika Bungeni.
![]() |
| Mbunge Ahmed Al Tibi |
Ahmed al-Tibi ambaye amekuwa mbunge tangu mwaka 1999, mara kadhaa amekuwa akilishutumu bunge hilo kuwa ni la kibaguzi na lisilo na utu.
Al Tibi pia ni kiongozi wa chama cha Arab Movement for Change (Ta'al).
Serikali ya Israel kupitia kamati ya sheria imepeleka bungeni muswada wa sheria utakapiga marufuku upigaji wa Adhana kwa kutumia vipaza sauti.

