MHUBIRI maarufu duniani Dr Zakir Naik amefiwa na baba yake aitwaye Abdulkarim Naik siku ya jumapili huko Mumbai nchini India.
![]() |
| Abdul karim Naik |
Taarifa zinasema Dr Zakir Naik hakuweza kuhudhuria katika mazishi ya baba yake kwa khofu ya kukamatwa na serikali ya India kwa shutuma kadhaa.
Serikali ya India inamuona Dr zakir kama mchochezi na mtu anayehimiza ugaidi duniani na kuleta vurugu katika jamii ya waislamu kutokana na mahubiri yake.
![]() |
| Dr Zakir Naik |
Kwa sasa Dr Zakir yupo nchini Malaysia na anatarajiwa kwenda kuhani muda wowote msiba wa baba yake nchini India. Dr Zakir ndiye mmiliki wa televisheni ya satalaiti ya Peace TV.
Baba yake alizaliwa mwaka 1928 huko Ratnagiri katika pwani ya Maharashtra.
Mwenyezi Mungu amsamehe makosa yake na alifanye kaburi lake kuwa moja ya Mabustani ya peponi.

