Mwenyekiti wa chama cha kijamii na demokrasia (Social Democratic Party) cha Uswisi Christian Levrat, amependekeza Uislamu kutambulishwa kama dini rasmi nchini.
Katika pendekezo lake, Levrat alisema, ‘‘Endapo Uislamu utatambulishwa kama rasmi, viongozi na walimu wa kidini watapokewa vizuri zaidi na jamii nchini Uswisi.’’
Maelezo ya Levrat pia yalipewa nafasi kubwa kwenye taarifa za gazeti la 20 Minuten.
Katika taarifa hizo, kuliandaliwa hoja na maoni kuhusiana na swali la ‘‘Je, Uislamu unapaswa kutambulishwa kama dini rasmi nchini Uswisi?’’
