Mussa alishiriki mashindano hayo akiwa amehifadhi juzuu 30 pamoja na washiriki wengine kutoka nchi mbalimbali.
![]() |
| Mussa daudi |
Mussa alikuwa ni mshiriki pekee kutoka Indonesia na ndiye aliyekuwa na umri mdogo zaidi kati ya washiriki wote waliokuwepo.
Japo hakushinda nafasi ya kwanza Mussa alipewa heshma ya juu kutokana na umri wake mdogo. Alisoma vizuri Qurani japo kuna matamshi hayakutoka vizuri kutokana umri wake kuwa mdogo sana kuweza kutamka baadhi ya matamko kwa ufasaha zaidi.
Musa anayefahamika kama 'Musa Hafidh' amezaliwa mwaka 2008. Mbali ya kuhifadhi Qurani pia anahifadhi hadith na tayari amehifadhi kitabu cha Imam Nawawiy cha Arubain Nawawiy. Akiwa na umri wa mika 5 na nusu tayri alishahifadhi juzuu 29.
![]() |
| Akiwa na familia yake |
Pia ndiye anayetambulika katika nchi ya Indonesia kama mtu aliyewahi kutokea kuhifadhi Qurani yote akiwa na umri mdogo.


