Aidha sambamba na visomo kwa ajili ya Sheikh Muhammad pia kutatumika nafasi hiyo kutawadhwa rasmi kwa Mudir mpya Sheikh Samir Sadiq pamoja Naib Mudir Sheikh Rashid Bakar,
| Mudir Sheikh Samir (kulia) pamoja na Naib wake Sheikh Rashid |
Sheikh Muhammad Bakar aliyekuwa Mudir wa Mahdi(chuo kikuu) Shamsul Maarif ya Tanga alifariki dunia usiku wa Jumatatu ya tarehe 7 mwezi wa Machi mwaka huu jiji Dar es Salaam.
Shekh muhammad Abubakar alizaliwa mwaka 1943 katika kijiji cha Doda wilaya ya mkinga mkoani tanga.
Alianza kusoma masomo ya dini tangu utotoni mwake kwa mwalimu Nabahani barabara ya sita ngamiani tanga mwanzoni mwa miaka ya hamsini.
Mwaka 1956 alikabidhiwa kwa sheikh Muhammad Ayubu akiwa tayari amekwishakhitimu Qur ani.
Wakati wa uhai wake alisema kwamba alipofika kwa sheikh Muhammad Ayubu alisikilizwa Qurani Suratul Baqara na Sheikh Ayubu aliridhika na usomaji wake kiasi cha siku hiyo hiyo alimkabidhi darsa la watoto wanaojifunza qur ani.
اللهم اغفر له، وارحمه