Saturday, 16 April 2016

IMAM WA MSIKITI WA MTUME MUHAMMADﷺ AFARIKI NA KUZIKWA LEO

Imam wa Msikiti wa Mtume Muhammad Masjid Nabaw uliko madina Sheikh Dr. Muhammad Ayyub ibn Muhammad Yusuf ibn Sulaiman `Umar محمد أيوب بن محمد يوسف بن سليمان عمر‎ amefariki leo alfajiri akiwa na umri wa miaka 65.

Sheikh Muhammad alisaliwa swala ya Jeneza wakati wa Adhuhuri na kuzikwa katika Makaburi ya Baqee.

Shekh alizaliwa mwaka 1372H(1952/1953) huko Mji wa Makkah.
Alijifunza kusoma na kuhifadhi Qurani akiwa na umri wa miaka 12 kwa Sheikh Daghistan na Khaleel ibn 'Sheikh Abdulrahman Al-Qari' katika msikiti wa Bin Ladin ulioko Makkah.
Alisoma tafsiri ya Qurani, Sayansi ya Qurani kutoka masheikh kadhaa wakiwemo Sheikh Muhammad Sayyed Tantawi, Sheikh Abdulaziz Mohammed Othman, Sheikh Akram Dhiya Al-Amri, Sheikh Muhammad Al-Amin Al-Shiqiti na Sheikh Abdul Mohsen Al-Abbad.


Ameacha wake wawili na watoto watano.