Sheikh Samir ametangazwa kushika nafasi hiyo kutokana na kifo cha aliyekuwa Mudir Sheikh Muhammad Bakar aliyefariki siku ya Jumatatu usiku jijini Dar es Salaam na kuzikwa Tanga Jumatano hii.
| Mudir Mpya wa Shamsul Maarif Sheikh Samir Sadiq |
Sheikh Samir Sadiq kwa muda wote alikuwa ndiye Naib Mudir wa Mahdi Shamsul Maarif.
| Mushrif Ustaadh Rashid Bakar |
Wengi wa wanafunzi na waalimu wa chuo hicho kutoka matawi mbalimbali ya chuo hicho nchini Tanzania wamefurahishwa kwa Sheikh Samir kuwa Mudir wa Shamsul Maarif.
Blogu ya Ahbaabur Rasuul inampongeza na kumtakia taufiq katika majukumu mazito aliyopewa.