Mwili wake umesafirishwa kwa ndege ukiambatana na baadhi ya wanafamilia na watu wa karibu wapatao 12.
Sheikh atazikwa kesho wakati wa alasiri katika viwanja vya Mahdi(chuo kikuu) Shamsul Maarif mtaa wa duga jijini Tanga.
Wageni mbalimbali kutoka sehemu kadhaa za ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kuhudhuria mazishi hayo.