Baba Massimo Biancalani na Alessandro Carmignani walitangaza wiki iliyopita kuwaruhusu kusali waislamu ndani ya kanisa baada ya parokia yao kuwakaribisha wakimbizi 18 waislamu.
![]() |
| Waislamu wakisali ndani ya kanisa |
"Sioni ni jinsi gani tatizo, tunaweza kuwatia ugumu kufanya ibada zao", alisema na kuongeza, "Mtu yeyote akitaka kuja kusali Kanisani anakaribishwa na hata kama wanataka kwenda sehemu nyingine wanaruhusiwa kufanya hivyo".
Lakini Askofu Mkuu Fausto Tardelli alisema mpango huo ni hatua ya mbali ambayo inaweza kuhatarisha na kuharibu kuwaunganisha wakimbizi hao katika jamii.
Alisema kuwapa misaada na kuwakaribisha haina maana kuwapatia nafasi katika Kanisa kufanya ibada zao. Kuna maeneo bora sahihi zaidi yanapatikana.
Pamoja na kupinga kwa Askofu mkuu wa Kanisa hilo Makuhani wa kanisa hilo wamepinga vikali kauli ya Askofu na kutaka wakimbizi hao waendelee kufanya ibada zao
kanisani hapo na kutaka Parokia zingine ziige mfano wao.
JE, uislamu unasemaje juu ya kusali ndani ya kanisa?
Fuatilia hapa hapa katika Blogu yako Ahbaabur Rasuul kupata majibu.
