Thursday, 6 March 2014

MWANAMUZIKI KATY PERRY ATOA KIDANI KILICHOANDIKWA الله ALLAH KATIKA VIDEO YA WIMBO WAKE MPYA

Baada ya kupigiwa kelele mwanamuziki wa kike wa POP wa marekani Katy Perry ameondosha kidani cha mkufu kilichokuwa na jina la الله Allah katika video ya wimbo wake mpya wa 'Dark Horse'.

katika video hiyo iliyotengenezwa kwa sura ya Misri ya kale na katy akionekana kama Malkia Cleopatra ndipo alijitokeza mtu aliyevaa kidani cha dhahabu kilichoandikwa الله Allah. 

Baada ya kuonekana video hiyo katika mtandao wa Youtube, viongozi wa jumuiya za kiislamu nchini Marekani walikusanya saini zaidi ya 60,000 kutaka kuondolewa video hiyo katika youtube.

Baada ya malalamiko hayo ya video hiyo iliyoangaliwa na watu milioni 40 katika wiki yake ya kwanza, mwanamuziki huyo aliamua kuifanyia uhariri (editing) kwa kuondoa picha ya kidani kilichoandikwa الله Allah.


Pich a yakushoto ndio muonekano wa awali na kulia ndio muonekano wa sasa