Thursday, 13 February 2014

RAIS WA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI AAPA KUKABILIANA NA ANT BALAKA

Rais wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Catherine Samba Panza, ameapa kuwa atapambana na wapiganaji wa Kikristo wa Ant-Balaka ambao walihusika na mashambulio ya hivi karibuni dhidi ya Waislamu katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui.

Rais Samba-Panza amesema waasi hao, wamepoteza mwelekeo na hawana dhamira yoyote. Amesema wapiganaji hao ambao walikuwa watetezi wa jamii, wamegeuka na kuwa wauaji na waporaji.

Maelfu ya Waislamu wameukimbia mji huo na kukimbilia nchi jirani ya Cameroon.

Jamhuri ya Afrika ya Kati imetumbukia kwenye machafuko ya umwagaji damu ambapo Wakristo wanawashambulia na kuwaua Waislamu tangu mwaka uliopita.

Catherine Samba Panza