Hatua hiyo ya Hormuud kufunga huduma za intaneti kwenye simu za mikononi mjini Mogadishu imekuja chini ya wiki moja baada ya Al Shabaab kuwakamata wafanyakazi 16 wa kampuni hiyo katika mji wa Jilib mkoani Jubba ya Kati, akiwemo meneja wa tawi, Mohamud Haji Salad.
Hata hivyo, wanamgambo hao wameripotiwa kuruhusu kurudi kwa huduma ya intaneti kwenye simu za mikononi katika mikoa ya Jubba ya Kati na Chini siku ya Alhamisi, kwa mujibu wa Redio RBC.
![]() |
| Kampuni ya simu ya Hormuud Telecom |
