Prince Khaled Al-Faisal.
Prince Khaled Al-Faisal alipokea ripoti hiyo kutoka kwa mwenyekiti wa kamati kuu ya Hijja Hisham bin Abdulrahman Al-Faleh.
![]() |
Vijana waliojitolea wakiwa Maji kwa Waumini |
Prince Khaled alishukuru mashirika ya serikali na mashirika yasiyo ya serikali yaliyojitolea kuwahudumia mamilioni ya mahujaji msimu wa mwezi wa ramadhani.
Waumini wapatao milioni 3 watokao nje ya nchi na milioni 2 watokao ndani ya Saudi Arabia walizuru Msikiti wa Makkah kwa ajili ya Ibada ndani ya Ramadhani ya mwaka huu.
Mpango huo wa kimkakati ulitekelezwa na kamati inayojumuisha mashirika kama vile wizara ya mambo ya ndani, afya, masuala ya Kiislam, ulinzi wa kiraia na mashirika mengine ya sekta binafsi.