Tuesday, 15 August 2017

MAHUJAJI 31 WAMEFARIKI SAUDI ARABIA

Jarida la serikali la Saudia Arabia limetangaza kuwa mahujaji 31 wameripotiwa kufariki Jumapili .

Hakuna taarifa zaidi zilizotolewa kuhusu sababu zilizopelekea maafa hayo.
Jarida hilo la "Saudi Press Agency" limesema kuwa watu waliofariki ni raia wa kigeni.

Mahujaji zaidi ya  620,000  wameshawasili nchini Saudia Arabia Agosti 12 kwa ajili ya kutekeleza ibada ya Hijja.