Mnamo Januari 3, Ihan aliapishwa kama mjumbe wa bunge la Baraza la Wawakilishi katika Jimbo la Minnesota na hivyo kuwa mwanamke wa kwanza Mwislamu Marekani kushika wadhifa huo.
Ilhan ambaye anawakilisha eneo la House District 60B la Minnesota, ameweka historia kama Msomali-Mmarekani kuchaguliwa kama mbunge nchini Marekani.
Wawili hao ni wanachama wa chama cha Democratic na Ellison hivi sasa anawania kuwa mwenyekiti Kamati ya Kitaifa ya Chama cha Democratic.
Ilhan Omar mwenye umri wa miaka 34 aliambatana na mumewe aliyekuwa amevaa kanzu, kofia na koti walibeba msahafu mkubwa kwa ajili ya kula kiapo kwa Ilhani.
