Mashindano hayo yalianza rasmi siku ya Jumatano katika Ukumbi Mkubwa wa Swala wa Imam Khomeini MA na yamemalizika leo Mei 17.
![]() |
| Rajai akiwa na zawadi yake |
Rajai Ayoub alifanikiwa kupita katika mchujo wa washiriki 57 waliochuana kutoka nchi mbalimbali duniani na kuwa miongoni wa sita bora waliopambana kumpata mshindi wa kwanza.
| Washiriki |
Nafasi ya nne ilichukuliwa na Syed Abbas Ali kutoka nchi ya Ujerumani na nafasi ya tano ilichukuliwa na Mustafa Ali kutoka Uholanzi.
![]() |
| Palipofanyikia mashindano |
Aidha katika upande wa kuhifadhi nafasi ya kwanza ilichukuliwa na Mojtaba Fard Fani ambaye nae ni raia wa Iran.
Nafasi ya pili na ya tatu ilichukuliwa na Abdul Aziz Ahmed kutoka Misri na Muhammad Ali Abdullah kutoka Australia.
Nafasi ya nne ilichukuliwa na Khalid Sankari from kutoka Ivory Coast na Muhammad Taha Hassan kutoka Niger.
Nchi 70 zilituma wawakilishi wao katika mashindano hayo ambayo kauli mbiu yake ni 'Kitabu Kimoja Umma Moja'..

