Ahlam Saeed alikuwa ameenda katika duka moja huko Shepherd’s Bush ambapo mwanaume huyo alianza kumkejeli mbele ya wanawe wawili.
![]() |
| Mbaguzi wa dini |
Mwanamume huyo ameripotiwa kutumia maneno ya ubaguzi aliposema, "Hii ni nchi ya kikristo,tupo katika dunia ya magharibi."
Bi Ahlam alianza maisha yake Uingereza tangu alipokuwa na umri wa miaka 2,na alianza kuvalia Niqab akiwa na miaka 22.
Mwanzoni mbaguzi huyo wa dini hakujua kama Ahlam anajua lugha ya kiingereza na kuendelea kumkejeli.
