Wanasheria walipiga kura kuondoa kifungu katika Mswada wa Sheria ya Ndoa kinachomtaka mume katika ndoa ya kimila kumweleza mkewe kabla ya kuoa mwanamke mwingine. Baadhi ya wanawake wanawake walionesha kuchukizwa kwao na marekebisho hayo kwa kutoka nje ya bunge.
Mswada huo pia ulitoa uamuzi kwamba ndoa zote zinapaswa kusajiliwa na kuweka kiwango cha chini cha umri wa ndoa, kuzuia watoto, hususan wasichana, dhidi ya kuolewa mapema.
Hata hivyo, kiongozi wa wengi Aden Duale, alichukulia suala hilo pamoja na kifungu cha usajili, akisema kitaathiri ndoa za Kiislamu ambazo hazihitaji usajili.
"Katika jimbo lililopanuka ninaloishi, watu wawili wanaweza kuamua kuoana msikitini na wanachukuliwa kama ndoa, Kutosajili hakutengui ndoa", aliongeza.
Katika dini ya Uislamu mwanaume amepewa ruhusa ya kuoa wanawake wanne tu.
![]() |
| Bunge la Kenya |
