Wanafunzi hao waligomba kulala shuleni na vyuoni mwao baada ya tukio hilo katika shule ya Federal Government iliyoko mjini Buni Yadi, katika jimbo la Yobe Jumanne.
“Wanafunzi wengi katika shule za mabweni wameondoka na kwenda makwao baada ya kupashwa habari kuhusu shambulizi la Buni Yadi,” Yunusa Ahmed anayeishi katika mji mkuu wa Damaturu aliambia AFP.
Mwanawe wa kiume Ahmed ni mwanafunzi katika Government Secondary School na amerejea nyumbani kwao pamoja na wenzake. “Walienda shuleni Jumatano lakini wamerudi nyumbani kwani hawataki kulala shuleni humo kutokana na hofu ya kushambuliwa na Boko Haram,” Ahmed alisema.
Kundi la Boko Haram linapinga masomo ya kigeni na imeteketeza mamia ya shule katika mapigano yake ya miaka minne na nusu yanayolenga kubuni jimbo la kiislamu kaskazini mwa Nigeria. Jina “Boko Haram” kwa Kihausa lamaanisha “Elimu ya Kigeni ni dhambi”.
Mwezi Oktoba mwaka jana maafisa wa Serikali katika jimbo la Yobe walisema wapiganaji wa kundi hilo waliteketeza shule 209, na kusababisha hasara ya kiasi cha dola 15.6 milioni za Marekani.
Mashambulizi hayo yanaathiri sekta ya elimu katika eneo hilo ambalo tayari liko nyuma katika nyanja za maendeleo likilinganishwa na maeneo mengine nchini Nigeria.
Akihutubia taifa kupitia runinga Jumatano jioni, Rais Goodluck Jonathan alisema wanafunzi hao waliuawa kikatili.
![]() |
| Boko Haram |
