Mesut Özil ambaye siku chache zilizopita alichaguliwa mchezaji bora wa Arsenal msimu huu, alisambaza picha alizopiga Makkah kwenye akaunti yake ya mtandao wa jamii wa Twitter na Instagram.
Maelfu ya mashabiki wa Mesut Özil wanaomfuatilia kwenye mitandao ya jamii walivutiwa mno na picha hizo alizosambaza mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid.
![]() |
| Mbele ya Al Qa'aba |
Kiungo wa Timu ya Arsenal Mesut Özil ametumia muda wake wa mapumziko baada ya kwisha kwa ligi za ulaya kwenda Makkah, Saudi Arabia kwa ajili ya kufanya Ibada ya Umrah.
Özil aliweka picha yake akiwa mbele ya Al qa'aba kupitia akaunti yake ya Instagram.
