Tuesday, 25 March 2014

MAHAKAMA YAAMURU WAFUASI 529 WA MORSI WAHUKUMIWE KIFO NCHINI MISRI

Mahakama moja mjini Minya, Misri, imetoa adhabu ya kifo kwa wafuasi na wanachama 529 wa harakati ya Ikhwanul Muslimin walikokuwa wakikabiliwa na mashtaka ya mauaji na kuvuruga amani.

Hukumu hiyo imelaaniwa na chama cha wanasheria nchini humo ambacho kimesema jeshi la Misri limerudisha udikteta ulioangushwa na wananchi mwaka 2011. 

Maandamano yamefanyika nje ya mahakama hiyo punde baada ya hukumu hiyo kutolewa.  
Mahakama imesema wafuasi hao wa Ikhwan wamehusika na mauaji dhidi ya maafisa wa usalama pamoja na kutatiza amani na utulivu ndani ya nchi.

Wafuasi wa Morsi wakilia nje ya mahakama baada ya hukumu kutolewa